Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Simba walitaka nipate kadi, wanipe IST" - Kabwili

Jumatatu , 27th Jan , 2020

Mlinda mlango wa klabu ya Yanga, Ramadhan Kabwili ametoa tuhuma nzito kuwa aliwahi kufuatwa na uongozi wa klabu ya Simba wakitaka atafute kadi ili asicheze mchezo wa watani na wampatie gari aina ya IST.

Ramadhan Kabwili

Kabwili amesema hayo alipokuwa akihojiwa katika kipindi cha Kipenga Xtra cha East Africa Radio, Jumatatu, Januari 27, 2020 ambapo amesema kuwa tukio hilo lilitokea wakati Yanga ikiwa na kocha Mwinyi Zahera.

Amesema kuwa siku hiyo Yanga ilikuwa inaelekea kucheza na JKT Tanzania na yeye alikuwa na kadi mbili za njano, hivyo Simba walimfuata na kumuambia kuwa atafute kadi moja ya njano ili akose mchezo uliokuwa unafuatia wa watani wa jadi huku wakimuahidi kumpa IST mpya, wakiamini kuwa angekaa Klaus Kindoki golini wangemfunga kirahisi.

Katika mchezo huo dhidi ya JKT Tanzania, Yanga ilipoteza kwa kufungwa bao 1-0 ambapo Ramadhan Kabwili ndiye alikuwa golikipa wa Yanga siku hiyo.

Aidha Kabwili amesema kuwa kwa sasa ahitaji meneja yoyote atakayemtafutia timu ya Tanzania akitamani meneja ambaye atamtafutia timu Ulaya, "mimi nataka meneja ambaye atanipeleka kucheza soka la Ulaya, sitaki meneja wa kunichezesha hapa nchini kwa sababu kama ni hapa nchini sasa hivi nipo katika klabu kubwa Tanzania na inashinda mataji".

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea