Jumapili , 10th Dec , 2017

Klabu ya soka ya Simba SC leo imefanya uzinduzi wa tawi jipya la Kibaha mkoani Pwani, ikiwa ni sehemu ya kuwaweka karibu wanachama wake wa maeneo hayo. 

Uzinduzi wa tawi hilo umefanywa na Mkuu wa Idara ya habari ya klabu hiyo Haji Sunday Manara na kuhudhuriwa na wanachama na mashabiki wa Simba wa Kibaha na matawi ya karibu.

Jumapili ya wiki iliyopita Simba iliingia rasmi kwenye mfumo mpya Wa uendeshaji wa klabu kutoka mfumo wa wanachama na kwenda kwenye mfumo wa hisa ambapo zabuni ya kuwekeza alishinda mfanyabiashaaa na shabiki wa klabu hiyo Mohammed Dewji ‘Mo’.

Pia vinara hao wa ligi kuu soka Tanzania Bara wamethibitisha kuwa kocha mkuu wa timu hiyo Mcameroon Joseph Omog atarejea nchini siku yoyote ndani ya wiki ijayo.

Omog alikwenda nchini kwao kwa mapumziko baada ya ligi kusimama ambapo mazoezi ya klabu hiyo yalianza jumatatu ya wiki hii chini ya kocha msaidizi Masoud Juma kwenye uwanja wa Polisi Kurasini.