Wachezaji wa timu zote wakigombea mpira
Magoli ya Simba SC katika mchezo huo uliopigwa jioni ya leo Oktoba 17, 2021 jijini Gaborone yamefungwa na nahodha wa kikosi hicho John Bocco dakika ya pili na sita kipindi cha kwanza.
Mchezo wa mkondo wa pili utapigwa jijini Dar es salaam kwenye dimba la Benjamin Mkapa wiki mbili zijazo. Mshindi wa jumla wa michezo hii miwili atafuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.