Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Simba 'yamtoa sadaka' Blagnon

Jumatatu , 16th Jan , 2017

Mshambuliaji wa kimataifa wa Ivory Coast anayeichezea klabu ya wekundu wa Msimbazi Simba, Fredrick Blagnon amepelekwa kwa mkopo katika klabu ya Muscat ya nchini Oman kwa miezi 6.

Fredrick Blagnon

 

Klabu ya Simba imeweka wazi kuwa mshambuliaji huyo atakwenda nchini Oman kwenye klabu ya Muscat kwa muda wa miezi sita kwa ajili ya kulinda kiwango chake na baada ya hapo atarejea Msimbazi endapo hakutakuwa na makubaliano tofauti.

Tangu asajiliwe kikosin hapo, Blangnon amekuwa hana nafasi ya uhakika katika kikosi cha kwanza hali ambayo baadaye ilipelekea kuwekwa benchi moja kwa moja na kocha Mcameroon, Joseph Omog licha ya kusumbuliwa pia na majeraha ya mara kwa mara.

Katika mechi za ligi kuu alizoichezea Simba, amefanikiwa kufunga bao moja pekee, huku akiwa hajacheza mechi hata moja tangu kuanza kwa mzunguko wa pili wa ligi, na hata kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi.

Simba imekuwa ikihaha kupata 'mtambo wa mabao' tangu iachane wa Hamis Kiiza, kiasi cha kusajili washambualiaji kadhaa wa kimataifa msimu huu akiwemo Laudit Mavugo na Fredrick Blagnon, lakini bado hawajakidhi mahitaji, na mabao mengi yamekuwa yakifungwa kupitia viungo.

Hali hiyo imeilazimu kuongeza washambuliaji wa kitanzania katika dirisha dogo la usajili ambao ni Juma Luizio kutoka Zesco ya Zambia na Pastory Athanas kutoka Stand United, ambao wameua kabisa ndoto za Blagnon kupata namba hata ya ziada klabuni hapo.

Simba inakipiga na Mtibwa Sugar, JUmatano ya Januari 18 mjini Morogoro, na tayari imekwishaondoka Dar s Salaam kwa ajili ya mechi hiyo.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea