Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Sports Countdown leo, Raducanu bilionea kijana

Jumanne , 14th Sep , 2021

'Sports Countdown' ya leo Septemba 14, 2021 inakupitisha kuzihesabu zile stori sita klai za kimichezo, Emma Raducanu awa bilionea baada ya ushindi wa kombe la michuano ya US Open, Edinson Cavani, Ng'olo Kane, Christian Pulisic, Aguero na Ansumane Fati kukosa mchezo wa UEFA Champions League

Mshindi wa michuano ya Tennis US Open, Emma Raducan akiwa ameshikilia kombe lake.

6 - Ni wiki ambazo mshambuliaji tegemezi wa klabu ya Azam, Prince Dube Mpumelelo anatazamiwa kuwa nje ya uwanja kujiunguza baada ya kufanyiwa upasuaji tarehe 9 Septemba mwaka huu katika Hospitali ya Vicent Pelloti jijini Cape Town, Afrika kusini na kufanikiwa kurejea nchini salama Alfajiri ya Jana Septemba 13.

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu ya Azam, Zacharia Thabiti amesema Dube alikuwa anapata maumivu makali kwenye maeneo ya chini ya kitovu kushoto pindi akijaribu kukimbia kwa kasi hivyo wanaimani kubwa tatizo hilo litapona na Dube kurejea kwenye utimamu wake wa kawaida.

Mbali na taarifa ya Dube, Zacharia Thabit amethibitisha kuwa, mchezo wao wa marudio wa hatua ya awali ya mtoano kuwania kufuzu Makundi ya kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Horseed ya Somalia utachezwa kwenye uwanja wa Chamazi na sio Uhuru tena, na hii ni mara baada ya Horseed wenye kuchagua hvyo.

5 - Ni idadi ya timu alizozichezea Cedric Ceballos kwenye ligi ya kikapu nchini Marekani NBA kabla ya kustaafu miaka 10 iliyopita. Timu hizo ni Phoenix Suns, Los Angeles Lakers, Dallas Mavericks, Detroit Pistons na Miami Heat.

Cedric Ceballos alizua taharuki juu ya afya yake nchini Marekani baada ya wengi kuwa na hali ya sintofahamu. Cedric amevunja ukimya usiku wa kuamkia leo kupitia akaunti yake ya IG kwa kupost picha ikionesha anatumia vifaa maalum vya kupumulia na akithibitisha kuwa amepona Covid-19 baada ya kuwa hoi kwenye chumba cha uangalizi maalum ICU kwa siku 10.

4 - Ni siku zilizopita tokea Mjumbe wa bodi ya wakurugenzi ya kampuni ya klabu ya Simba, Zacharia Hans Pope afariki dunia Septemba 10, 2021 alipokuwa anapatiwa matibabu kwenye hospitali ya Agha Khan jijini Dar es Salaam.

Baada ya kuagwa jana na watu mbalimbali kwenye viwanja vya Karimjee, Posta jijini Dar, Zacharia Hans Pope anataraji kuagwa tena Asubuhi ya leo na Familia yake pekee na baadae mchana Mwili wake utasafarishwa kuelekea Mkoani Iringa ambapo mazishi yake yatafanyika huko, Eneo la Kihesa Mkimbizi.

Aendelee kupumzika kwa Amani. Amen.

3 - Ni idadi ya miaka iliyopota tokea bondia Anthony Joshua wa England ampige bondia Andy Ruiz JR wa Mexico na kufanikiwa kutetea mikanda yake ya pambano la uzito wa juu wa Dunia ya WBA, IBF, WBO na IBO katika pambano lililofanyika mji wa Diriyah, Saudi Arabia 2019.

Mbabe huyo wa kutoa dozi neno amesema kwasasa amefikia kwenye kiwango cha juu katika maisha yake ya masumbwi lakini ili azidi kuweka historia zaidi na zaidi basi hana budi kupigana na mabondia wenye uwezo wa juu na kutamka kutaka kuzichapa na Muingereza mwenzake Tyson Fury baada ya pambano lake na Oleksandor Usyk wa Ukraine Septemba 25 mwaka huu kwenye ulingo uliopo kwenye uwanja wa Tottenham Hotspurs, England na kutaraji kuwa na watazamaji 60,000 walioketi.

Anthony Joshua na Oleksandor Usyk watapigana kugombania mikanda ya uzito wa juu wa Dunia ya WBA, IBF, WBO na IBO.

2 - Ni idadi ya michezo itakayoanza kucheza usiku wa mapema ya leo Septemba 14, 2021 katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya kwa msimu mpya wa mwaka 2021-2022, michezo hiyo ni Young Boys (Uswizi) vs Manchester United (England) kutoka kundi F na Sevilla vs Salzburg (Austria) kutoka kundi G ambazo zote zitachezwa saa 1:45 Usiku wa leo.

Manchester United wanataraji kumkosa mshambuliaje wake Edinson Cavani aliyepata maumivu ya kifundo cha mguu na kutaraji kuwa nje kwa wiki moja au zaidi ilhali CR7 amesafiri na kikosi hadi Uswizi tayari kwa ajili ya kuleta mabalaa.

Michezo mingine itakayochezwa usiku wa leo ni 6 amabayo yote itachezwa saa 4:00 usiku. Kundi E Barcelona (Hispania) itacheza na Bayern Munich (Ujerumani) bila ya Washambuliaji wake Martin Braithwait aliyefanyiwa upasuaji wa goti,  Ansu Fati na Sergio Aguero wakusumbuliwa na kifundo cha mguu. Dynamo Kyiv (Ukraine) itakipiga na Benifica (Ureno).

Kundi E, Villareal dhidi ya Atalanta. Kundi F, Lille itachuana na Wolfsburg. Kundi H, Mabingwa watetezi Chelsea (England) watacheza na Zenit St.Petersburg bila kiungo bora wa Ulaya Ng'olo Kante na Christian Pulisic wanaosumbuliwa na maumivu ya kifundo cha mguu ilhali Malmo (Sweeden) itacheza na Juventus.

1 - Ni nafasi anayoishikilia mwanadada, Emma Raducanu katika viwango vya ubora vya mchezo wa tennis nchini England na kumpiku Johanna Konta baada ya Raducanu kumfunga Leylah Fernandez wiki iliyopita na kuwa bingwa wa US Open kwa mara ya kwanza.

Baada ya ubingwa huo wa kihistoria kwa Raducanu, mwanadada huyo mwenye miaka 18 amepanda rasmi kwenye viwango vya ubora vya mchezo huo kutoka nafasi ya 150 hadi sasa nafasi ya 23 duniani na ya kwanza England kwa upande wa wanawake na makamu bingwa wa US Open, Leylah mwenye miaka 19 na yeye amepanda kutoka nafasi ya 73 Duniani hadi nafasi ya 28 kwasasa baada ya kufika fainali hiyo.

Emma Raducanu amejizolea paundi Milion 1.3 za England sawa za bilioni 300 na milioni 600 za Kitanzania kwa kuwa bingwa wa michuano ya US Open.

HABARI ZAIDI

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya