Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tarimba azipania Simba na Yanga, SportPesa Cup

Jumanne , 22nd Jan , 2019

Michuano ya SportPesa Super Cup mwaka 2019, inatarajia kuzinduliwa leo katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam kwa michezo miwili kupigwa.

Abasi Tarimba

Mchezo wa kwanza wa leo utakuwa ni kati ya Singida United na Bandari ya Kenya, majira ya saa 8:00 mchana huku Yanga ikiwakaribisha Kariobang Sharks ya hukohuko Kenya huku katika mchezo wa pili wa saa 10:00 jioni.

Kuelekea ufunguzi wa michuano hiyo, Mkurugenzi wa Uendeshaji wa SportPesa nchini, Abbas Tarimba, amevitaka klabu za Simba na Yanga kutumia vikosi vya kwanza ili kuepusha aibu ambayo imekuwa zikiionesha katika misimu miwili iliyopita.

"Imekuwa ni utamaduni wetu, Samahani nitatumia neno 'kudharau' haya mashindano, awamu hii hatutaki utani, tunataka kombe libaki nyumbani kwa maana kila siku limekuwa likienda nchi jirani. Tunavitaka vilabu vyote vya hapa nyumbani kuhakikisha vinafanya vizuri", amesema Tarimba.

"Nilivyokuwa naingia hapa nilikutana na kocha wa Yanga, nikamsisitiza kuwa hatutaki utani katika mashindano ya mwaka huu", ameongeza.

Awali, michuano hii ilikuwa ikifanyika mwezi Juni baada ya ligi kumalizika lakini Tarimba amesema kuwa imekuwa ikilalamikiwa na vilabu hasa vya Tanzania kuwa inapofika mwishoni mwa msimu, wachezaji wengi mikataba yao huwa inamalizika kwahiyo kukosa fursa ya kushiriki. 

Pia ameitaja sababu nyingine kuwa ni klabu hizo kutokuwa na muda mrefu wa maandalizi kutokana na ligi kumalizika, tofauti na timu za Kenya ambazo katika kipindi hicho ligi yao inakuwa inaendelea.

Mshindi wa michuano hiyo atajinyakulia kitita cha Dola za Kimarekani 30,000 ambazo ni takribani shilingi milioni 65 za Kitanzania, huku mshindi wa pili akijinyakulia Dola 10,000, wa tatu atapata Dola 7,500 na mshindi wa nne atapata Dola 5,000.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea