Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Temeke Heroes na Portland zamgusa Rais

Jumatatu , 23rd Jul , 2018

Ushindani uliooneshwa kwenye mechi ya robo fainali ya Sprite Bball Kings kati ya Temeke Heroes dhidi ya Portland, ulimgusa Rais wa shirikisho la mpira wa Kikapu nchini (TBF), Phares Magesa ambaye alikuwepo kwenye uwanja wa taifa wa ndani kushuhudia mechi hizo.

Timu za Temeke Heroes (jezi nyeupe) na Portland (kijani) kwenye mechi yao ya robo fainali.

Mechi hiyo ambayo ilimalizika kwa Portland kushinda kwa pointi 83 dhidi ya 70 za Temeke heroes ilishuhudiwa ikianza kwa ushindani mkubwa ambapo quater ya kwanza hadi ya tatu hazikuweza kutabiri mshindi hadi mechi ilipoingia quarter ya 4 ambapo Portland walijihakikishia kushinda.

Akifanya mahojiano maalum na www.eatv.tv baada ya mechi 4 za robo fainali, zilizofanyika kwenye uwanja wa ndani wa taifa, Magesa alisema mchezo wa Temeke heroes na Portland ni kivutio tosha cha mashabiki kuja uwanjani kwenye mechi zinazofuata kwani watakuwa wanaamini kuna burudani tofauti na timu zingepoteza kwa pointi nyingi.

''Kiukweli ushindani ni mkubwa sana. Mechi ya mwisho ilikuwa kama fainali huwezi kujua mshindi mpaka 'querter' ya mwisho. Vijana wameonesha viwango vikubwa sana na hiki ndio TBF tunataka ili mchezo huu uendelee kuwavutia mashabiki lazima ushindani wa aina hii uwepo'' - alisema.

Rais wa TBF Phares Magesa (kulia) akiwa na katibu wake Mike Mwita (kushoto) wakifuatilia mechi za robo fainali ya Sprite Bball Kings.

Magesa pia alitoa pongezi kwa waandaaji ambao ni East Africa Television LTD na wadhamini wa mashindano ambao ni kinywaji cha Sprite akisema huo ni mfano tu kwa wadau wengine kuona umuhimu wa mchezo huo na kujitokeza kuweka nguvu zao.

Bingwa wa michuano hii atajinyakulia kitita cha shilingi milioni 10 huku mshindi wa pili akitunza shilingi milioni 3 na mchezaji bora wa mashindano 'MVP' akihifadhi kiasi cha shilingi milioni 2. Droo ya mechi za nusu fainali leo, itaoneshwa moja kwa moja kwenye 5Sports na kusikika kupitia 'The Cruise' 

HABARI ZAIDI

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi