Katika salamu hizo za rambirambi, Malinzi amewapa pole familia ya marehemu, ndugu jamaa na marafiki, FUFA kufuatia msiba Dhaira, na kusema TFF ipo pamoja nao katika kipindi hiki cha maombelezo.
Dhaira alifariki jana Jumapili kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa Kansa
Wakati wa uhai wake Dhaira aliwahi kuidakia timu ya Taifa ya Uganda ‘The Cranes’ na kuvichezea vilabu vya Express FC, URA (Uganda), AS Vita (Congo DR), Simba SC (Tanzania) na klabu ya BV Vestmannaeyjar ya Iceland.