Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tuchel amwagia sifa Olivier Giroud

Jumatano , 24th Feb , 2021

Kocha wa Chelsea, Thomas Tuchel amemwagia sifa mshambuliaji wake Olivier Giroud baada ya nyota huyo kufunga bao moja na la ushindi dhidi ya timu ngumu ya Atletico Madrid kwenye mchezo wa mtoano mkondo wa kwanza hatua ya 16 bora klabu bingwa barani Ulaya uliochezwa usiku wa jana.

Kocha wa Chelsea, Thomas Tuchel akimpongeza mshambuliaje wake Olivier Giroud baada ya kufunga bao na kumfanyia mabadiliko usiku wa jana.

Tuchel amesema “Ukimuona kwenye mazoezi ya kila siku, huwezi kushangazwa na alichokifanya. Mwili wake upo kwenye utayari na utimamu wa hali ya juu. Anafanya mazoezi kama kijana wa miaka 20 au 24”.

“Ni mtu mwenye umakini sana na utani awapo mazoezini. Muda wote ana mawazo chanya jambo ambalo ni muhimu sana kwenye timu. Akianza au akitokea benchi bado ana ubora kitu ambacho ni kizuri”.

Olivier Giroud mwenye umri wa miaka 34, alifunga bao hilo dakika ya 68 kwa 'Tik taka' na kuwashangaza wengi kutokana na uzuri wa bao hilo na kuifanya timu yake kupata ushindi na faida ya bao 1-0 ugenini kwenye mchezo ulichezwa Bucahrest nchini Romania.

Olivier Giroud akiifungia bao timu yake ya Chelsea usiku wa jana dhid ya Atletico Madrid.

Bao hilo ni la 6 kwa Giroud kwenye michuano hiyo msimu huu ikiwa ni mengi zaidi kwenye msimu mmoja tokea kucheza michuano hiyo, lakini akifikisha mabao 11 katika michezo 22 katika michuano yote msimu huu akiwa na Chelsea.

Kwa upande wa kocha wa Atletico Madrid, Diego Simeone amekiri ubora wa Chelsea kwenye mashambulizi na kusema imewalazimu kucheza kwa kujilinda zaidi jambo hata lililopelekea kucheza bila kupiga shuti hata moja lililolenga lango tokea wafanya hivyo mara mwaka 2017 dhidi ya Juventus.

“Ilikuwa ni mechi ngumu, hakuna timu iliyopata nafasi nyingi za kufunga. Lakini pia ilikuwa ngumu kutokana na ushambuliaji wao kwasababu wanawachezaji wenye nguvu na ubora”.

Kipigo hiko kinaifanya Atletico Madrid kusalia na ushindi mmoja tu katika michezo yake 5 ya mwisho, akifungwa mchezo wa pili mfululizo na kutoa sare mbili.

Wawili hao wanataraji kurudiana mapema mwezi ujao kwenye dimba la Stamford bridge jijini London nchini England.

 

HABARI ZAIDI

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera