Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tujifunze kitu katika safari ya Samatta na Msuva

Jumatano , 8th Jan , 2020

Ili ukacheze Ulaya sio kitu rahisi, haswa ukiwa unatokea mataifa ambayo kwenye ramani ya soka hayapo hata kwenye nafasi 100 bora. Pongezi kwa Simon Msuva kutoka Yanga mpaka Difaâ Hassani El Jadidi na sasa anaelekea Panathinaikos ya Ugiriki.

Mbwana Samatta akiwa na Simon Msuva kwenye moja ya mechi za timu ya taifa.

Ili ufike Ulaya inabidi ukacheze ligi ambazo zinatazamwa zaidi na mawakala pamoja na Scouts wa vilabu vikubwa duniani. Kwa Afrika moja ya ligi hizo ni ya Afrika Kusini, Misri, Morocco, Cameroon, Nigeria, Ivory Coast, DR Congo na kwingineko ambako tayari wameshaliteka soko la Ulaya kwa kuwa na wachezaji wengi.

Msuva na Samatta nadhani walitafuta taarifa sahihi mapema, juu ya jinsi gani wanaweza kutimiza ndoto za kucheza Ulaya ama walifanyakazi na watu Smart na wakawapa njia za kupita ikiwemo kucheza ligi zinazofuatiliwa zaidi.

Leo ndoto zao zinazidi kutimia lakini wakiwa wamebeba mzigo mkubwa wa taifa.  Je kama wadau wa soka Mashabiki, Watangazaji, Wachambuzi na Mamlaka kama TFF, BMT, na Wizara  mpaka Serikali Kuu kwa Ujumla tunajua kama tunatakiwa kutumia hii fursa kuweka mazingira wezeshi kwa wengine kufuata nyayo hizi ?

Wakati mzuri ndio huu ambao bado Samatta na Msuva wanacheza ili utambulisho uwe rahisi kwamba natoka anapotokea mfungaji bora wa Mabingwa wa Ubelgiji KRC Genk au natokea anapotoka Winga wa Benfica ya Ureno anayecheza kwa mkopo Panathinaikos ya Ugiriki.

Endapo tutajisahau kutumia huu mlango uliopo wazi kwasasa, ukija kujifunga tutajuta. Kucheza Ulaya ukiwa unatokea Tanzania sio kazi rahisi kama tunavyodhani hata Wanyama alipotoka Tanzania alipita mataifa kadhaa ndio akafika White Hart Lane.

Kupitia kipindi cha Shabiki On Saturday kinachoruka kupitia East Africa Television, Msuva alikutana na Wanyama na alijikita kumuuliza namna ya kupenya na kuwavutia makocha wa Ulaya. Wanyama alimpa elimu nzuri siku hiyo na bila shaka ilimjenga kufika alipofika leo.

Tuungane tusaidie wengine wajipenyeze kwenye njia za kina Msuva na Samatta ili hii kazi iwe rahisi kadri miaka inavyokwenda. Hongera Simon Msuva kwa Deal hii, hakika umelifanya taifa liinuke.
 

HABARI ZAIDI

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya