Jumatano , 2nd Mar , 2022

Gwiji wa zamani wa klabu ya Ac Milan na timu ya taifa ya Ukraine Andriy Shevchenko ametoa ujumbe wa kusisitiza amani kwa nchi ya Ukraine kwenye mchezo wa nusu fainali ya kwanza wa kombe la Coppa Italia baina ya Ac Milan dhidi ya Inter Milan kwenye uwanja wa San Siro

Nyota wa zamani wa Ac Milan Andriy Shevchenko

Shevchenko mwenye umri wa miaka 45 ambaye ni mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa dunia kwa mwaka 2004 (Ballon D’or), video yake fupi ilioneshwa kabla ya kuanza kwa mchezo huo maarufu kama Derby Della Madonnina.

“marafiki zangu kutoka italia, tafadhali pazeni sauti zenu, watu wa Ukraine wanataka amani kwa sababu amani haina mipaka” amesema Shevchenko

Mchezo huo uliomalizika kwa suluhu ambapo sasa watarudiana tena mnamo jumatano ya April 20 huku nusu fainali ya pili ikitarajiwa kuchezwa leo baina ya klabu ya Fiorentina watakapowakaribisha kibibi kizee cha Turin Juventus majira ya 23:00 usiku katika uwanja wa Stadio Artemio Franchi