Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ubingwa Kombe la Mapinduzi, Bocco afichua siri

Jumapili , 15th Jan , 2017

Nahodha wa Azam FC, John Bocco ‘Adebayor’, amefichua siri ya timu hiyo kutwaa ubingwa wa Kombe la Mapinduzi mwaka huu, na kusema kuwa hivi sasa wanahamishia nguvu zao zote kwenye michezo ya ligi kuu Tanzania Bara.

Nahodha wa Azam, John Bocco (Katikati) akiongoza wachezaji wenzake wakati wakiingia na kombe la jijini Dar es Salaam kutoka Zanzibar

Bocco amesema kikubwa kilichowapa ushindi ni pamoja na sapoti kutoka uongozi wao ambao uliwatimizia kila kitu walichohitaji, lakini pia ushirikiano pamoja na kuwasikiliza walimu.

“Naamini hatukuwa na papara, tuliweza kutulia, tuliweza kupata sapoti kutoka kwa viongozi wetu pamoja na mashabiki wetu na kuwasikiliza walimu wetu ndio kama hivi tunamshukuru Mungu tumeanza kidogo kupata mafanikio.” Amesema Bocco

Alisema kuwa wana furaha kubwa kutwaa taji hilo huku akiwapongeza wachezaji wenzake kwa namna walivyojituma hadi kufikia fainali na kupata mafanikio hayo.

“Kwanza tunamshukuru Mungu kwa ushindi huu ni matokeo mazuri kwetu tumeweza kutwaa Kombe la Mapinduzi, kikubwa nawaomba wachezaji wenzangu tuweze kuweka jitihada katika michezo ya Ligi Kuu ianyokuja, tuwasikilize walimu wetu nini wanachotueleza ili tuweze kufanya vizuri na hata michuano ya kimataifa,” alisema.

Naye kipa bora wa michuano hiyo, Aishi Manula, ambaye amecheza mechi zote bila kufungwa bao, amesema anajisikia faraja sana kuweza kutwaa tuzo hiyo huku akiwaambia mashabiki kuwa ubingwa huo unaamanisha kuwa wao wamerudi kwenye ubora wao na kuonyesha kama ni timu kubwa.

“Napenda kumshukuru Mungu, kwa hiki ambacho wamenipatia na pia kuishukuru timu nzima kwa ujumla kwa kuweza kucheza vizuri hasa mabeki wameweza kunilinda vizuri na tumeweza kumaliza mashindano haya bila kuruhusu bao, pia ni kitu kizuri kwa sababu hili linakuwa kombe la pili kuchukua bila kuruhusu bao, kwanza Kagame tuliweza kulichukua bila kuruhusu bao na hili la Mapinduzi kwa hiyo ni kitu kizuri,” alisema.

HABARI ZAIDI

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita