Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ufaransa kutumia uzoefu kuwanyanyasa Croatia ?

Alhamisi , 12th Jul , 2018

Ufaransa ambao wameshawahi kutwaa ubingwa wa dunia mara moja, watacheza fainali ya kombe la dunia dhidi ya Croatia, taifa ambalo ndio litakuwa linacheza hatua hiyo kwa mara ya kwanza.

Bao la Mario Mandžukić (mwenye jezi nyeusi) alilofunga dakika ya 109 na kuipeleka fainali timu yake.

Hii imekuja baada ya Croatia kuwaondoa England katika mchezo wa nusu fainali kwa kipigo cha mabao 2-0, katika mchezo ambao umechezwa kwa dakika 120. Bao la Mario Mandžukić dakika ya 109 liliungana na bao la kusawazisha la Ivan Perisic la dakika ya 68 na kulipoteza bao 1 la kutangulia la England lililofungwa na Kieran Trippier.

Mchezo wa fainali sasa unakutanisha mataifa mawili yenye historia tofauti, ambapo Ufaransa wanauzoefu zaidi wa kucheza hatua ya fainali wakiwa tayari wameshacheza mwaka 1998 na kutwaa ubingwa dhidi ya Brazil huku wakipoteza fainali ya mwaka 2006 dhidi ya Italia.

Kwa upande wa Croatia wao ni wageni wa hatua hiyo wakiwa ndio wamefika kwa mara ya kwanza. Wakiwa na kizazi cha dhahabu Croatia wamekuwa na safari imara kuanzia hatua ya makundi ambapo waliongoza kundi kwa kushinda mechi zao zote ikiwemo 3-0 dhidi ya Argentina.

Nayo timu ya taifa ya England imekuwa na bahati mbaya na hatua ya nusu fainali ikiwa imeshaondolewa katika nusu fainali 4 tofauti. Ilipoteza nusu fainali ya Euro 1968 dhidi ya Yugoslavia, ikapoteza nusu fainali kombe la dunia mwaka 1990 na Euro 1996 zote dhidi ya Ujerumani pamoja na ya leo dhidi ya Croatia.
 

HABARI ZAIDI

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera