Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wabishi Iceland wakiona wapigwa mkono na Ufaransa

Jumatatu , 4th Jul , 2016

Dunia jana ilishuhudia jumla ya magoli saba yakitinga nyavuni katika mchezo wa robo fainali ya mwisho baina ya wenyeji Ufaransa ambao walikuwa wakivaana na timu ngumu ya Iceland mchezo uliopigwa katika dimba la Stade de France.

Wachezaji wa timu ya taifa ya Ufaransa wakiwashukuru mashabiki wao.

Katika mchezo huo wenyeji wa michuano ya mataifa ya Ulaya Euro 2016 inayoendelea nchini Ufaransa timu ya taifa ya Ufaransa usiku wa kuamkia hii leo wamefanikiwa kukata tiketi ya kucheza nusu fainali ya michuano hiyo baada ya kuichapa timu ya Iceland kwa jumla ya magoli 5-2.

Kwa ushindi huo sasa timu ya taifa ya Ufaransa inaungana na timu nyingine za Ureno, Wales, mabingwa wa dunia Ujerumani katika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo ambapo michezo yake itapigwa katikati ya juma hili.

Katika mchezo huo Ufaransa ambayo ilicheza mchezo huo kwa kasi na kudhamiria ushindi huo mapema magoli yake yalifungwa na Olivier Giroud aliyepachika mawili 2 katika dakika ya 13 na 59, lingine likifungwa dakika ya 20 na kiungo mshambuliaji wa timu hiyo Paul Pogba, na dakika 2 baadaye kunako dakika ya 45 Dimitri Payet akapachika lingine huku Antonie Griezmann akifunga dakika ya 43 .

Magoli yakufutia machozi kwa upande wa Iceland yamepachikwa na Kolbeinn Sigthorsson katika dakika ya 58 na dakika ya 84 Birkir Bjarnason alifunga bao la pili lakufutia machozi.

Nusu fainali ya michuano hiyo itapigwa katikati ya wiki hii ambapo Ureno wao watavaana na timu ya Wales huku wenyeji Ufaransa watakuwa na kibarua kizito mbele ya mabingwa wa dunia timu ya taifa ya Ujerumani.

HABARI ZAIDI

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera