Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Walikotokea Flying Dribblers mpaka fainali

Jumatatu , 6th Aug , 2018

Baada ya kuishia hatua ya nusu fainali mwaka uliopita, timu ya Flying Dribblers, mwaka huu imekuwa timu ya kwanza kutinga fainali ya michuano ya Kikapu ya Sprite Bball Kings baada ya kushinda mechi zao mbili kwenye 'best of three' za nusu fainali dhidi ya Team Kiza.

Timu ya Flying Dribblers wenye jezi nyeusi kwenye mchezo wao wa game 2 dhidi ya Team Kiza (nyeupe).

Safari ya Flying Dribblers kwenda fainali ilianza kwenye hatua ya mchujo ambapo ilicheza na timu ya Kurasini Worriors na kushinda kwa pointi 37 kwa 9. Katika mchezo huo uliopigwa kwenye uwanja wa JK Park, mchezaji Habirmana Mayeye alifunga pointi 11.

Baada ya kushinda mchujo, timu ya Flying Deribblers ilitinga 16 bora na kucheza na Ukonga Hitman kwenye uwanja wa Air Wing Ukonga ambapo ilishinda kwa pointi 87 kwa 63 na kutinga robo fainali. Katika mchezo huo mchezaji Baraka Mopele alikuwa kinara kwa kufunga pointi 36.

Kwenye robo fainali Flying Dribblers walicheza na Water Institute kwenye uwanja wa Bandari Kurasini ambapo walishinda kwa pointi 100 kwa 64, hivyo kujikatia tiketi ya nusu fainali. Katika mchezo huo Baraka Mopele alikuwa nyota kwa kufunga pointi 25.

Katika nusu fainali ambayo imechezwa kwa mtindo wa 'best of three' Flying Dribblers imeshuhudiwa ikimaliza kazi mapema tu baada ya kushinda 'game 1' na 'game 2' hivyo kuepuka kwenda 'game 3' dhidi ya wapinzani wao Team Kiza.

Flying Dribblers walishinda 'game 1' kwa pointi  84 kwa 70 za Team Kiza ambapo mchezaji Habirmana Mayeye alikuwa kinara kwa kufunga pointi 26, Assist 1 na rebound 4. Katika game 2 iliyopigwa Jumamosi Agosti 4 Flying Dribblers wakashinda tena kwa pointi 69 kwa 63 mara hii Baraka Mopele akifunga pointi 21 rebound 3 na Assist 1.

Flying Dribblers sasa tayari wameshajihakikishia milioni 3 kati ya 15 zinazotolewa kama zawadi na wadhamini ambao ni kinywaji cha Sprite ambapo bingwa ataondoka na milioni 10, milioni 3 kwa makamu bingwa na milioni 2 kwa mchezaji bora MVP. 

Flying Dribblers watajua mpinzani wao wa fainali siku ya Jumatano Agosti 8 ambapo Mchenga Bball Stars watacheza na Portland kwenye game 3 baada ya game 1 na game 2 kumalizika kwa kila timu kushinda mechi moja.
 

HABARI ZAIDI

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria