Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wanachama wa Yanga waitwa kumalizana na jengo

Jumanne , 18th Jun , 2019

Baada ya mapema leo viongozi wa Yanga kuoneshwa eneo la kujenga uwanja wao huko Kigamboni na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda, uongozi wa Yanga umewaita wanachama wake.

Jengo la Yanga

Kupitia taarifa iliyotolewa usiku huu, uongozi wa klabu ya Yanga umetoa wito rasmi kwa wadau na wapenzi wa klabu hiyo ambao wangependa kufanya ukarabati wa vyumba katika Jengo la Makao makuu ya klabu hiyo lililopo mitaa ya Twiga na Jangwani jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Yanga, Dkt. Mshindo Msolla, amesema Kamati ya utendaji iliyoketi mwishoni mwa wiki imebariki kuanza kwa zoezi hilo kupitia wadau wenye mapenzi mema na klabu hiyo, ili kuwawezesha wachezaji kuishi katika jengi hilo. 

“Kwenye hafla ya Kubwa Kuliko nililieleza hili, nashukuru Kamati ya Utendaji imelipitisha, sasa rasmi tunawaalika wadau, ikiwa ni mwanachama mmoja, Tawi la Yanga, Kundi la WhatsApp au hata kampuni kufika klabuni kuanzia Alhamisi, ambapo tutakuwa tumeanisha gharama za ukarabati wa kila chumba hivyo watachagua kulingana na uwezo wao,” amesema Dkt. Msolla.

Amesema kukarabatiwa kwa vyumba katika Jengo la Yanga, kutasaidia kuondoa gharama kubwa ambazo timu hiyo imekuwa ikizitumia kwenye hoteli wakati wa kambi za mazoezi ya kawaida hasa timu inapokuwa jijini Dar es Salaam. 

“Tutatoa nafasi kwa vyumba kupewa majina ya wadau waliofanya ukarabati, mfano kama ni tawi la Makao Makuu, basi Chumba kitaitwa Makao Makuu kama watapenda, hivyo hii ni nafasi nyingine wa wadau wetu kusaidia maendeleo ya klabu yao kwa kuiepusha na gharama zinazoweza kuepukika,” alisema.

Jengo la Yanga lina jumla ya vyumba 28 pamoja na maeneo mengine muhimu ikiwemo eneo la kufanyia mazoezi ya Ndani (gym) ambayo pia inahitaji ukarabati mkubwa pamoja na kuwekwa vifaa vya kisasa.
 

HABARI ZAIDI

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya