Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watanzania walia na dili la Samatta

Jumatatu , 20th Jan , 2020

Ni takribani siku ya tano sasa tangu zilipoibuka tetesi juu ya mshambuliaji wa Genk na timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars', Mbwana Samatta kuwaniwa na klabu ya Aston Villa.

Mbwana Samatta

Watanzania wanasubiri kwa hamu kubwa kusikia taarifa ya utambulisho wa Samatta hasa katika mitandao yake ya kijamii, ambako Watanzania wamezidi kuifuatilia. Hilo linajidhihirisha hata katika 'comments' zilizopo katika kurasa za Twitter na Instagram za klabu hiyo.

Taarifa hizo ziliripotiwa na mitandao yote mikubwa nchini Uingereza na Ubelgiji, Januari 17 kuwa Aston Villa imemmulika Samatta kuwa ni mbadala katika safu ya ushambuliaji baada ya kuumia kwa mshambuliaji wao tegemeo, Wesley Moraes, ambapo dau lililotajwa kwenye uhamisho huo ni Pauni milioni 8.5.

Siku iliyofuata Januari 18 ziliripotiwa taarifa kuwa Genk imeshamalizana na Aston Villa na Samatta ametua Jijini Birmingham nchini Uingereza kwa ajili ya vipimo vya afya na kukamilisha dili hilo.

Kinachoendelea hivi sasa ni kwamba Samatta amekamilisha vipimo vya afya na klabu hiyo na kinachosubiriwa ni ukamilishwaji wa masuala machache ikiwemo vibali vya kazi. Januari 18, mtangazaji maarufu wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Salim Kikeke alithibitisha kuwa kila kitu kimekwenda sawa na kinachosubiriwa ni utambulisho wake.

Aston Villa itawakaribisha Watford katika uwanja wake wa nyumbani, kesho Jumanne katika mchezo wa ligi kuu nchini Uingereza. Kuna uwezekano mkubwa wa kukosekana kwa Samatta kwenye mchezo huo, kwani mpaka sasa hajatambulishwa rasmi.

HABARI ZAIDI

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya