Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watu watatu wauawa kwa risasi

Jumamosi , 9th Mar , 2019

Watu watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wameuawa kwa kupigwa risasi na askari polisi katika maeneo ya Murungushi Igogo jijini mwanza wakati wakijaribu kurushiana risasi na askari polisi waliokua doria.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Jumanne Muliro.

Kamanda wa Polisi mkoani humo Jumanne Muliro, amesema tukio hilo lilitokea eneo hilo la Igogo jirani na ghala la kiwanda cha Avant linalotumika kuhifadhi bidhaa za vipuli vya magari na vifaa vya ujenzi, huku majambazi wengine wakifanikiwa kukimbia baada ya kukaidi amri ya kujisalimisha.

Muliro ameongeza kuwa majambazi hao waliouawa walikuwa na silaha aina ya 'Shortgun' iliyokuwa na risasi 4, mapanga matatu, nondo moja, mkasi mkubwa wa kuvunjia milango na makufuli na pia funguo nyingi zinazotumika kufungulia milango, makufuli na droo za ofisi na maghala.

Kwa mujibu wa Kamanda Muliro, majambazi hao waliofariki wana umri kati ya miaka 30 hadi 35 na miili yao imehifadhiwa katika hospitali ya mkoa wa Mwanza Sekou Toure kwa uchunguzi na utambuzi zaidi.

Pia ameeleza kuwa watuhumiwa wengine wa ujambazi waliotoroka eneo la tukio wanasakwa kwa udi na uvumba ili watiwe nguvuni na jeshi la polisi.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea