Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga ni kama gari ya maiti - Julio

Jumapili , 26th Feb , 2017

Kocha mwenye maneno mengi ambaye hivi karibuni alitangaza kustaafu kufundisha mpira nchini Jamhuri Kihwelo 'Julio' ameibuka na kuiponda Yanga kuwa haikuwa na uwezo wa kuifunga Simba, huku akiifananisha na gari ya maiti

Julio ambaye amewahi kuichezea Simba na baadaye kuifundisha kwa nyakati tofauti, ametoa kauli hiyo mara baada ya Simba kuishushia kipigo Yanga cha mabao 2-1 katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa katika dimba la Taifa Dar es Salaam.

Kocha huyo ambaye alitangaza kustaafu akiwa na timu ya Mwadui FC kwa madai ya kuchoshwa na waamuzi wa Tanzania, amesema ameamua kuunganisha nguvu kutoka kwa baadhi ya wachezaji wa zamani wa Simba akiwemo Zamoyoni Mogella, kuunda kundi la hamasa kwa wachezaji wa Simba ili kuhakikiksha Simba inaifunga Yanga na kuchukukua ubingwa msimu huu.

Amesema kabla na wakati wa mchezo wa jana, yeye na wenzake wamefanya kazi kubwa ya kuwatia hamasa wachezaji na hata wakati wa mapumziko, waliingia vyumbani na kuwatia hamasa wachezaji ya kupambana na ndiyo maana timu kipindi cha pili ilibadilika na kucheza kwa ari kubwa.

Mashabiki wa Yanga wakiwa wamekaa kwa huzuni mara baada ya timu yao kupigwa bao 2-1 na timu ya Simba katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania bara

"Sisi kazi yetu ni kuwahamasisha wachezaji, hatumuingilii mwalimu, mwalimu anafanya kazi yake, lakini sisi tunawaambia wachezaji wanapaswa kupambana, ndiyo kazi tuliyoamua kuifanya kuelekea mchezo huu hata wakati wa mapumziko, kwa kazi tuliyofanya Yanga wasingeweza kutufunga, na mimi tangu nimeanza kufundisha mpira sijawahi kufungwa na Yanga, .. Yanga ni kama gari ya maiti, ya kwanza kuondoka, ya mwisho kurudi, ndiyo maana nasema hawa ni kama mwembe wetu wa uwani, wakati wowote tunautikisa unadodosha maembe" Amesema Julio.

Pia Julio amewapongeza makocha wa Simba kwa kazi kubwa waliyoifanya ya kuusoma mchezo na kufanya mabadiliko yenye tija, pamoja na kuwajenga wachezaji kisaikolojia, ambapo licha ya kuwa nyuma, pamoja na mchezaji wao mmoja kutolewa, walionesha kutokata tamaa.

Wachezaji wa Simba wakishangilia bao la kusawadhisha liliwekwa kimyani na mshambuliaji Laudit Mavugo

HABARI ZAIDI

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita