Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga yaibuka na sakata la Kabwili

Jumatano , 29th Jan , 2020

Uongozi wa klabu ya Yanga umeibuka na sakata la tuhuma za upangaji matokeo zilizoibuliwa na mlinda mlango, Ramadhani Kabwili alipokuwa akihojiwa na kipindi cha Kipenga Xtra cha East Africa Radio.

Ramadhani Kabwili

Katika mahijiano hayo yaliyofanyika Jumatatu, Januari 27, Kabwili alisema kuwa alishawishiwa na moja ya kiongozi wa klabu ya Simba kuwa atafute kadi ya njano katika mchezo mmoja kabla ya mchezo wa watani ili atimize kadi tatu na akose mchezo huo unaofuata, akimuahidi kumpa gari mpya aina ya IST.

Baada ya kauli hiyo, Shrikisho la Soka Tanzania TFF lilitoa taarifa ya kufuatilia suala hilo sambamba na klabu ya Simba, ambapo hii leo klabu ya Yanga imeibuka na kumkingia kifua mchezaji wao.

Akizungumzia tulio hilo, Afisa Habari wa Yanga, Hassan Bumbuli amesema kuwa wao kama klabu walilamikia tukio hilo mnamo Februari 12, 2019  na kocha Mwinyi Zahera, na kwamba alichokifanya Kabwili ni kuelezea historia ya tukio lenyewe lilivyokuwa.

"Kilichofanywa hapa na Kabwili ni kuelezea historia ya tukio hilo kwa uzoefu wake kwenye kucheza mechi kubwa kama ile na umri wake ni mdogo pamoja na changamoto ambazo alikutana nazo", amesema Bumbuli.

"Kwahiyo kwa sababu suala limekuwa hivyo na sisi tumemuita mchezaji wetu tukae naye na atueleze kinagaubaga nini kimetokea, tukusanye ushahidi wote na tuupeleke kwenye vyombo vinavyohusika", ameongeza.

Mtazamo wa wengi unatofautiana kuhusu suala hilo, wapo wanaosema kuwa Kabwili amekosea kulisema suala hilo katika chombo cha habari na badala yake angelipeleka TFF tena mapema zaidi na wapo wanaosema yupo sahihi kwa kuwa masuala nyeti kama hayo hayapaswi kufumbiwa macho katika soka.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala