Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga yakalia kuti kavu Kombe la Shirikisho Afrika

Jumanne , 26th Jul , 2016

Klabu ya Yanga ya Dar es salaam Tanzania leo imejiweka katika mazingira magumu zaidi ya kufuzu kuingia katika hatua ya nusu fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika baada ya kuchapwa bao 3-1 na Medeama ya nchini Ghana.

Mshambuliaji wa Yanga (Amiss Tambwe (Kushoto) akiwania mpira dhidi ya mchezaji wa Medeama

Mechi hiyo iliyopigwa katika dimba la Essipong Sports, imeshuhudia Yanga Ikionesha kandanda lisilo na matumaini, na kuwaruhusu wapinzani wao kutawala sehemu kubwa ya mchezo kwa kufanya mashambulizi yenye uhai zaidi.

Medeama wamefungua kitabu chao cha mabao mapema kabisa kwa kosakosa moja dakika ya 5 kabla ya kupata bao lao la kwanza kati ya dakika ya 7 kupitia kwa Daniel Amoah.

Yanga imeendelea kushambuliwa mashambulizi ambayo yalizaa penati kwa Medema, ambayo hata hivyo, Medeama walishindwa kuitumia vizuri penati hiyo ambayo iliokolewa kiustadi mkubwa na golikipa namba moja wa Yanga Deogratius Munis Dida, kabla ya kupata bao la pili kupitia kwa Abbas Mohammed dakika ya 23.

Yanga ilizinduka na kufanya mashambulizi yaliyozaa penati iliyotokana na mshambuliaji wa Yanga Chirwa kuangushwa katika eneo la hatari, na penati hiyo kufungwa kiufundi na Simon Msuva dakika ya 25.

Medeama walicharuka na kufanya mashambulizi ya mara kwa mara yaliyozaa bao la tatu dakika ya 36, kupitia kwa Abbas Mohammed tena na hadi kipindi cha kwanza kinamalizika, Medeama ilikuwa inaongoza kwa mabao 3-1.

Matokeo hayo hayakubalika hadi dakika 90 zinamalizika, licha ya timu zote kuonesha uwezo wa mashambulizi ya hapa na pale.

Mechi hii ni ya marudiano ambapo katika mchezo wa kwanza kati ya Yanga na Medeama uliopigwa katika dimba la Taifa Dar es salaam, timu hizo zilitoka sare ya kufungana bao 1-1.

Kwa matokeo haya, Yanga inabaki na pointi yake 1 katika Kundi A, huku Medeama wakifikisha pointi 5 sawa na MO Bejaia, huku TP Mazembe ikongoza kwa kuwa na pointi 7.

TP Mazemba na MO Bejaia wanakutana kesho nchini DRC.

HABARI ZAIDI

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria