Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga,Azam mikononi mwa Wanyarwanda na Wasauzi

Ijumaa , 11th Mar , 2016

Kesho ndiyo kesho kwa miamba ya soka nchini Tanzania timu za Yanga na Azam na JKU zitakapokuwa katika viwanja tofauti kusaka alama tatu muhimu katika michezo ya kwanza ya hatua ya kwanza ya michuano ya vilabu barani Afrika.

Kikosi cha wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya klabu bingwa barani Afrika timu ya Yanga.

Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya kimataifa kwa ngazi ya vilabu barani Afrika michuano ya CAF timu za Azam FC na Yanga za Tanzania bara na JKU ya Zanzibar kesho wanashuka dimbani ugenini katika viwanja tofauti kusaka alama tatu muhimu katika michezo ya kwanza ya hatua ya kwanza ya michuano ya vilabu barani Afrika.

Azam fc wao wanacheza mchezo wa kombe la shirikisho barani Afrika dhidi ya wenyeji wao timu ya Bidvest Wist ya Afrika kusini huku maafande wa jeshi la kujenga uchumi visiwani Zanzibar JKU wao watakuwa Kampala Uganda kuvaana na majogoo wa huko timu ya Sports Club Villa katika mchezo wa kombe la Shirikisho.

Yanga ambao watavaana na wenyeji wao timu ya maafande wa jeshi la Rwanda APR hiyo kesho,ambapo mkuu wa idara ya habari ya timu hiyo Jerry Muro ametamba kuvunja mwiko wa kuishia raundi za awali na kwamba wamejiwekea malengo ya kusonga hatua za juu zaidi msimu huu.

Akiongea kwa kujiamini mno Jerry Muro ambaye husifika kwa tambo nyingi za majigambo ya kusisimua hasa wanapotupiana vijembe na mkuu wa idara ya habari ya wekundu wa msimbazi Simba Haji Manara amesema mipango hiyo ya timu hiyo kuvunja rekodi si kwa maneno bali ni ubora wa mafiga matatu ya klabu hiyo kuanzia kikosi cha wachezaji bora na benchi bora la ufundi, uongozi imara wa timu hiyo na tatu ni ushirikiano baina ya timu na umoja wa mashabiki.

Muro amesema watu wengi wamekuwa wakiibeza timu hiyo kwa kuwa mara kwa mara huhishia katika araundi za mwanzo lakini safari hii kwa mara ya kwanza anathibitisha kwa kauli yake kuwa kikosi bora walichonacho kwa sasa kikiongozwa na pacha watatu wajulikanao kama MTN akiwataja kwa mjina Msuva, Tambwe na Ngoma na wengineo wanauhakika wakuvuka raundi zote za awali na kutua katika hatua ya makundi msimu huu.

Akimalizia Jerry Muro amewaomba watanzania kuondoa tofauti zao za kiushabiki na kuelekeza dua zao zote kwa wawakilishi wote wa Tanzania katika michuano ya vilabu barani Afrika ili timu hizo ziweze kufanya vema katika michuano hiyo mikubwa barani Afrika kwa ngazi ya vilabu.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala