
Picha ya Mchezaji Zaki Anwari
Zaki alikuwa akiichezea timu ya taifa ya vijana ya Afghanistan na aliripotiwa kupoteza uhai wakati akijaribu kuokoa uhai wake baada ya ndege hiyo kupaa angani.
Tangu Taliban walipoteka nchi ya Afghanistan, maelfu ya watu wamejitokeza kwenye uwanja wa ndege wa Kabul, wakati ambapo nchi za Magharibi zinakimbilia kuhamisha raia wao na wenzao wa Afghanistan.