Ijumaa , 20th Aug , 2021

Mamlaka ya Afghanistan imethibitisha kuwa mwanasoka kijana Zaki Anwari (19) alifariki dunia baada ya kujaribu kuondoka nchini humo kwa kudandia ndege ya jeshi la Merekani USAF Boeing C-17 na kuanguka katika uwanja wa kimataifa wa Kabul.

Picha ya Mchezaji Zaki Anwari

Zaki alikuwa akiichezea timu ya taifa ya vijana ya Afghanistan na aliripotiwa kupoteza uhai wakati akijaribu kuokoa uhai wake baada ya ndege hiyo kupaa angani.

Tangu Taliban walipoteka nchi ya Afghanistan, maelfu ya watu wamejitokeza kwenye uwanja wa ndege wa Kabul, wakati ambapo nchi za Magharibi zinakimbilia kuhamisha raia wao na wenzao wa Afghanistan.