Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Zidane apewa listi ya 'mastaa' wa kutua Madrid

Jumanne , 12th Mar , 2019

Baada ya kocha Zinedine Zidane kurejea rasmi klabu ya Real Madrid kwa mtakaba wa miaka mitatu, Rais wa klabu amempa listi ya wachezaji wa kuanza nao katika usajili wa msimu ujao.

Rais wa Real Madrid, Florentino Perez (kushoto) akiwa na kocha Zinedine Zidane.

Akizungumza katika hali ya utani wakati wa utambulisho wa Zidane, Rais wa klabu, Florentino Perez amesema ana matumaini kuwa Zidane atakuwa ni daraja la kuwapata mstaa wa PSG, Kylian Mbappe na Neymar.

"Zidane ni Mfaransa, kwahiyo anaweza kufanya kitu fulani na Mbappe", amesema Perez na alipoulizwa ni nani atamchagua kumsajili kati ya Neymar na Mbappe, Perez akajibu "wote".

Real Madrid ilifikia uamuzi wa kumuondoa kocha, Santiago Solari kufuatia mlolongo wa kusuasua katika michuano mbalimbali, ambapo mpaka anaondoka, Real Madrid ilikua imesalia katika La Liga pekee ambapo inakamata nafasi ya tatu huku ikiondoshwa katika michuano ya Klabu Bingwa Ulaya na Copa del Rey.

Urejeo wa Zidane unaaminika kuwa unaweza kuwa sababu ya kuwavuta mastaa kutoka vilabu vikubwa barani Ulaya ambao wamekuwa wakihusishwa kujiunga na miamba hiyo, ni kwa sababu ya uhodari wa kocha huyo kuishi na wachezaji wake..

Licha ya Kylian Mbappe, mstaa wengine wanaohusishwa kujiunga na Real Madrid ni pamoja na Neymar, Eden Hazard, Christian Eriksen na Harry Kane.

Bonyeza hapa chini kutazama zaidi.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja