Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

George Mpole huru,amalizana na Geita Gold

Jumatano , 7th Dec , 2022

Klabu ya soka ya Geita Gold umefikia maridhiano ya kusitisha mkataba na aliyekuwa mchezaji wao George Enock Mpole kuanzia leo Disemba 7 ,2022.

Kupitia barua iliyovuja ya mshambuliaji huyo kusitishiwa mkataba ilisema,

 "Uongozi wa klabu ya Geita Gold, unakutaarifu rasmi ya kwamba mkataba wako wa ajira kati ya klabu na wewe (Mpole) umemalizika rasmi leo baada ya pande mbili kukubaliana na uko huru kujiunga na klabu yoyote kuanzia leo,"

"Tunachukua fursa hii pia kukushukuru kwa kazi, ushirikiano na utendaji mzuri uliouonyesha kwa klabu kwa kipindi chote tangu tumekuwa pamoja mpaka tulipokubaliana kusitisha mkataba wetu. Pia tunakutakia kila la kheri katika maisha yako ya mpira wa miguu," imesema taarifa hiyo.

Sakata la George Mpole na klabu yake limeanza kufukuta tangu Oktoba 13, mwaka huu baada ya mchezo wa raundi ya saba ambapo nyota huyo hakuungana na wenzake kwa maandalizi ya michezo iliyofuata.

Mpole hakuonekana kambini kwenye michezo mbalimbali ya timu hiyo kwa kile alichoeleza kuumwa na yuko nyumbani kwao mkoani Mbeya anatibiwa kwakuwa madaktari wa timu hiyo wameshindwa kumpa tiba huku baadhi ya taarifa zikidai mshambuliaji huyo anadai stahiki zake za mshahara wa mwezi wa 10.

HABARI ZAIDI

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera