
kikosi cha Simba
Kikosi kitaondoka kwa ndege maalumu ya kukodi itakayobeba wachezaji, benchi la ufundi viongozi na baadhi ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali hapa nchini.
Simba wanaamini kuwa iwapo watatumia usafiri wa ndege za kawaida ama wangepata changamoto za kuchelewa kufika au kuondoka huko na suala ambalo lingepelekea kuathiri maandalizi yao ya mechi ya marudiano.
Lakini mbali na kwenda na kurudi Angola kwa ndege ya kukodi, Simba imepanga kutua nchini humo siku moja kabla ya mechi, kwa maana ya Jumamosi asubuhi na jioni itafanya mazoezi katika Uwanja wa 11 de Novembro uliopo jijini Luanda ambao utatumika kwa mechi hiyo kesho yake, Jumapili, Oktoba 9 na baada tu ya mchezo huo, msafara wa Simba utapanda ndege kurejea Dar es Salaam kwa ajili ya kuanza maandalizi ya mechi itakayofuata.
Sababu kubwa iliyoufanya uongozi wa Simba kwa kushauriana na benchi la ufundi chini ya kocha Juma Mgunda kuamua timu hiyo isikae Angola kwa muda mrefu ni kuepuka hujuma za wenyeji ambazo ziawafanya wachezaji kuathirika kisaikolojia.