Akiwa mkoani Shinyanga IGP Sirro, amewaonya wananchi kuacha kujihusisha na vitendo vya imani za kishirikina, vinavyopelekea mauaji.
Aidha, IGP Sirro amemuagiza Kamishna wa Operesheni na Mafunzo Nchini, CP Liberatus Sabas, na Makamanda wote wa Mikoa ya Shinyanga, Geita, Kagera,Mwanza na Simiyu, kufanya operesheni ya pamoja itakayosaidia kukomesha vitendo vya mauaji nchini.