
Kocha mkuu wa timu ya Taifa Stars Etienne Ndayiragije
Taifa Stars ilihitaji ushindi ili iweze kusonga mbele katika hatua ya robo fainali. Guinea ilikuwa ya kwanza kupata bao kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 4 tu ya mchezo, lakini Taifa Stars walisawazisha dakika ya 29 kwa shuti la mbali nje ya box lililopigwa na Baraka Majogoro.
Stars ilichangamka zaidi katika kipindi cha pili na kufanikiwa kupata bao kunako dakika ya 69, lililofungwa na beki wa kushoto Edward Manyama, kufuatia kona iliyopigwa na Farid Mussa.
Kama ilivyo mwenye 'bahati habahatishi' Guinea walisawazisha goli kunako dakika 82 kwa bao lililofungwa na Victor Kantabadouna, ambalo lilipelekea ndoto za Stars kusonga mbele kutoweka kabisa, maana Stars alipaswa kupata matokeo ya ushindi tu, sare au matokeo mengine yasinge inufaisha.
Hatua ya robo fainali zinatarajiwa kuanza jumamosi tarehe 30/1/2021 kwa michezo miwili na kumalizika jumapili 31/1/2021 michezo miwili pia.
Ratiba Kamili
30/1/2021 Mali vs Congo
30/1/2021 DR Congo vs Cameroon
31/1/2021 Morocco vs Zambia
31/1/2021 Guinea vs Rwanda