Kushoto ni picha ya Rais Samia iliyowekwa kwenye jengo la Burj Khalifa na kulia nai Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa.
Taarifa hiyo ameitoa hii leo Machi 2, 2022, kupitia ukurasa wake wa Twitter na kusema kuwa utawala wa Dubai umeweka tangazo hilo kwa kutambua ziara ambayo Rais Samia Suluhu Hassan, aliyoifanya Dubai na utawala huo umeahidi kuendelea kuitangaza Tanzania kupitia jengo hilo maarufu.


