Baadhi ya wahamiaji haramu waliokamatwa
Akithibitisha kukamatwa kwa wahamiaji hao Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Uhamiaji mkoani Iringa Agnes Luziga, amesema raia hao wamekamatwa jana Machi 8, 2022, majira ya saa 1:00 jioni.
Luziga ameeleza kuwa jana jioni alipata taarifa kutoka kwa raia mwema kuwa kuna gari linasadikiwa kubeba wahamiaji haramu ambalo katika gari hilo kulikuwa na ‘seal’ ya TRA ambayo ilikuwa sio rahisi kwa mtu kugundua.
"Wahamiaji tuliowakamata ni raia wa Ethiopia wametokea Ethiopia kupitia mpaka wa Hororo-Taveta wakielekea nchini Afrika Kusini wakienda kutafuta maisha, hivyo taratibu za kuwafikisha mahakamani watuhumiwa hawa zinaendelea," amesema Agnes.






