Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky
Rais Zelensky alisema hayo katika mahojiano yake na majadiliano na viongozi wa mataifa yaliopiga hatua kubwa kidemokrasia na kuongeza kwamba iwapo Taifa lake lingefanikiwa kupata silaha hizo ambazo wameahidiwa wiki zijazo, zingesaidia kuokoa maisha ya maelfu ya watu.
"Hatma ya makumi ya maelfu ya wakaazi wa Mariupol ambao walipelekwa katika maeneo yanayodhibitiwa na Urusi haijulikani", amesema Zelensky.
Rais ameongeza kwamba uwezo wa mashambulizi ya Urusi katika maeneo ya Kharkiv, Donbasna Dnipropetrovsk umeongezekana hata kulenga makaazi ya raia.