(Mgombea wa Urais wa Yanga SC, Eng.Hersi Said akiwa na Farid Mussa)
"Kwa usajili wa ndani hatuna presha ya watu na tunaleta hawa kwa ajili kutetea ubingwa wetu na ushiriki wetu wa michuano ya kimataifa na tutasajili wachezaji 4 au 5 wa kimataifa tu huku wachezaji hao wamecheza katika ligi kuu ya Afrika Kusini, Ivory Coast, Angola pamoja na mmoja kutoka Afrika Mashariki na hatujataja majina yao kwa sababu wengine wana mikataba na vilabu vyao" amesema Manara.
Miongoni mwa wachezaji wanaodaiwa kukamilisha usajili wa kujiunga na Yanga SC kwa msimu ujao ni Stephane Aziz Ki na Lazarous Kambole.