
Kocha Mkuu wa Simba Queens, Sebastian Nkoma
Nkoma amesema lengo la kwanza ni kuhakikisha tunashinda na kuchukua ubingwa kuwapa furaha mashabiki wetu na kuweka historia ya kuwa timu ya kwanza Tanzania kushiriki Ligi ya Mabingwa Afrika.
“Kikosi kipo tayari morali kwa wachezaji ipo juu, tunajua mchezo utakuwa mgumu lakini tumejipanga kuhakikisha tunashinda ili kuchukua ubingwa,” amesema Nkoma.
Kwa upande wake mshambuliaji Aisha Juma amesema wao kama wachezaji wapo kamili ingawa wanafahamu mchezo utakuwa mgumu lakini lengo ni moja kuchukua ubingwa.
“Sisi tupo tayari tunajua mchezo utakuwa mgumu lakini tumejiandaa kushinda kikubwa tunahitaji mashabiki waje kwa wingi uwanjani kutupa sapoti,” amesema Joelle.