Arne Slot na Mohamed Salah
Winga huyo mwenye umri wa miaka 33 aliachwa nje ya kikosi kilichomenyana na Inter Milan kwenye Ligi ya Mabingwa siku ya Jumanne na kuondoka na ushindi wa goli 1-0
Akizungumza mjini Milan Jumatatu usiku, Slot aliongeza kuwa "hakuwa na fununu" ikiwa Salah, ambaye alitia saini mkataba mpya wa miaka miwili mwezi Aprili , angecheza mechi yake ya mwisho akiwa na Liverpool, lakini akaongeza kuwa "anaamini kwamba kuna uwezekano wa kurejea tena kwa ajili ya mchezaji".
Aliongeza kwa kusema "Kwa kawaida mimi ni mtulivu na mwenye adabu, lakini hiyo haimaanishi kuwa mimi ni dhaifu, Ikiwa mchezaji ana amri hizi kuhusu mambo mengi, basi ni kuhusu mimi na klabu kuguswa. Tuliitikia kwa njia ambayo unaweza kuona - hayupo hapa."
"Baada ya kesho tutaangalia hali ilivyo. Daima kuna uwezekano wa kurejea kwa mchezaji. Sijui - siwezi kujibu swali hilo kwa wakati huu."




