Klabu ya Lugalo ya Gofu kumuenzi Jenerali Galinoma

Mnadhimu Mkuu Wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania-JWTZ,Luteni Jenerali Mathew Mkingule (Upande wa kushoto) akimkabidhi zawadi mshindi wa jumla Nsajingwa Mwansasu (Upande wa kulia) Kwenye Hafla ya kufunga Shindano la kumuenzi aliyekuwa Mwenyekiti Wa klabu ya Lugalo Gofu Marehemu Brig.Jenerali Mstaafu Ernest John Galinoma "Galinoma Memorial Tournament" Lililofanyika Kwenye Klabu hiyo Dar es salaam.
Mnadhimu Mkuu Wa Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania-JWTZ,Luteni Jenerali Mathew Mkingule ameipongeza Klabu ya Gofu Ya Lugalo pamoja na familia kwa kuandaa shindano la "Galinoma Memorial Tournament" lililofanyika Kwenye Klabu hiyo Jijini Dar es salaam.