Ukwepaji wa kodi liwe jambo la aibu - Dkt. Nchemba
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema kuwa ipo haja kwa watoto wadogo kuanza kuelimishwa juu ya umuhimu wa kulipa kodi ili watoto wakue wakijua kwamba ukwepaji wa kodi ama upokeaji na utoaji wa rushwa ni jambo la aibu katika familia.

