Anayedai kugeuzwa msukule miezi 4, azungumza
Jeshi la polisi wilayani Magu mkoani Mwanza limemuokoa kwenye mikono ya wananchi wenye hasira kali Salome James, mkazi wa Kijiji cha Sato anayedaiwa kuwafanya misukule baadhi ya wakazi wa kijiji hicho na kuwatumikisha kwenye mashamba yake.