Radi yauwa mwanafunzi Kagera
Mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya sekondari Kabugaro iliyoko kata Nyakato katika halmashauri ya wilaya ya Bukoba mkoani Kagera amepoteza maisha baada ya kupigwa na radi akiwa shuleni, kufuatia mvua zilizonyesha asubuhi ya leo.