Kenya yasitisha safari za Uingereza
Shirika la Ndege la Kenya Airways limesitisha safari zake kuelekea Uingereza kufuatia mzozo wa kidiplomasia kati ya mataifa hayo mawili, hivyo watu wanaotaka kusafiri kwenye mataifa hayo wametakiwa kufikia tarehe tisa mwezi huu, kabla ya hatua hiyo kuanza kutekelezwa.