Real Madrid yapata pigo lingine kisa Covid-19
Mabingwa wa kihistoria wa michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya, klabu ya Real Madrid itamkosa mlinizi wake wa kati tegemeo Rafael Varane kwenye mchezo wa robo fainali ya kwanza dhidi ya Liverpool saa 4:00 leo usiku baada ya nyota huyo kukutwa na maambukizi ya Covid-19 asubuhi ya leo.