Uganda kuomboleza siku 14 kifo cha Magufuli
Rais Yoweri Museveni wa Uganda amesema nchi yake inaungana na Watanzania kuomboleza kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na kutangaza siku 14 za maombolezo ambapo bendera zote zitapepea nusu mlingoti.