Mwenyekiti Yanga akiri maji kuzidi unga
Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Dkt. Mshindo Msolla ametoa ufafanuzi juu ya mapato na matumizi ya klabu hiyo tangu uongozi wake ulipoingia madarakani, Juni 2019, huku akibainisha uwepo wa madeni ambayo wamerithi kutoka kwa uongozi uliopita.