Serikali yaeleza matokeo ya ujenzi wa viwanda 100
Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mwita Waitara, amesema mpaka sasa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wamewezesha ujenzi wa viwanda takribani 3000, tangu lilipotolewa agizo la ujenzi wa viwanda 100 katika kila Mkoa.