RC Makalla Aongoza Wananchi wa Arusha Kupiga Kura
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla, leo asubuhi Oktoba 29, 2025, ameongoza kwa vitendo zoezi la upigaji kura kwa kutimiza haki yake ya kikatiba ya kuchagua viongozi, huku akiwaasa wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki mchakato huo wa kidemokrasia.


