Wanaume waliosababisha kifo cha Lucy wakamatwa
Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limesema linawashikilia watuhumiwa wawili ambao ni John Peter (45) dereva na mkazi wa Manyire Wilayani Arumeru Mkoani Arusha na Jafari Shirima (62) dereva na Mkazi wa Singida kwa kusababisha ajali iliyopelekea kifo cha Lucy John (40) mkazi wa Manyire.