Wanawake vijijini Wanakosa Msaada wa Sheria
Serikali imekiri kuwa wanawake wengi wa vijijini wanakumbana na changamoto ya kupata msaada wa sheria na kusema Wizara ya Katiba na Sheria imeshapeleka mapendekezo ya kutunga sheria ya msaada wa kisheria utakaofanya wanawake wote kupata msaada huo.