'Mwanangu huna nidhamu' lilikuwa Dongo la MJ
Msanii Godfrey Tumaini maarufu kwa jina la Dudu baya, amefunguka juu ya wimbo ambao ulimpa umaarufu wa mwanangu huna nidhamu, na kusema wimbo huo lilikuwa dongo la Master Jay.
Akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio, Dudu baya alisema aliuandika wimbo huo baada ya kuchukizwa na kitendo cha Master Jay kumtupia pesa yake aliyompa ya kurekodi, baada ya kumjia juu kwa nini hawajerekodi kwa muda kama walivyokubaliana.