Marouf Tchakei amgalagaza Pacome tuzo mwezi Oktoba

Tchakei alionesha kiwango kizuri chenye mwendelezo kwa mwezi Oktoba akiwashinda Lusajo Mwaikenda wa Azam FC na Pacome Zouzoua wa Yanga, alioingia nao fainali katika mchakato wa tuzo za mwezi uliofanywa na Kamati ya tuzo za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Mshambuliaji wa timu ya Singida Black Stars Marouf Tchakei,amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Oktoba wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa mwaka 2024/25, huku Rachid Taoussi wa Azam FC akichaguliwa Kocha Bora wa ligi hiyo kwa mwezi huo.

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS