Mchezo KMC FC dhidi ya Simba SC kuchezwa Novemba 6
Bodi ya Ligi Tanzania (TPLB) imefanya maboresho ya ratiba ambapo mchezo wa Ligi Kuu namba 82 kati ya Simba dhidi ya KMC sasa utapigwa Jumatano, Novemba 6. Mchezo huo ulikuwa umepangwa kuchezwa Jumanne ya Novemba 5 katika Uwanja wa KMC.