Pinda atoa agizo fedha za mfuko wa barabara
Waziri mkuu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mizengo Pinda amewaagiza wakurugenzi na wakuu wa mikoa kuhakikisha sheria na kanuni za mfuko wa fedha za barabara zinafuatwa hasa kupitia ripoti ya kila robo mwaka ya matumizi ya mifuko wa barabara na kijiridhisha.
Mh. Pinda ameongeza kuwa ili kuepuka matumizi mabaya ya fedha ni lazima ripoti za kila robo mwaka za mapato na matumizi ziweze kuwasilishwa ili kuharakisha utekelezaji wa ujenzi wa barabara za halmashauri.